Isaiah 19:1-6
Unabii Kuhusu Misri
1 aNeno kuhusu Misri: Tazama, Bwana amepanda juu ya wingu liendalo kwa harakanaye anakuja Misri.
Sanamu za Misri zinatetemeka mbele yake,
nayo mioyo ya Wamisri inayeyuka ndani yao.
2 b“Nitamchochea Mmisri dhidi ya Mmisri,
ndugu atapigana dhidi ya ndugu,
jirani dhidi ya jirani,
mji dhidi ya mji,
ufalme dhidi ya ufalme.
3 cWamisri watakufa moyo,
na nitaibatilisha mipango yao.
Watatafuta ushauri kwa sanamu na kwa roho za waliokufa,
kwa waaguzi na kwa wale waongeao na mizimu.
4 dNitawatia Wamisri
mikononi mwa bwana mkatili
na mfalme mkali atatawala juu yao,”
asema Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote.
5 eMaji ya mito yatakauka,
chini ya mto kutakauka kwa jua.
6 fMifereji itanuka;
vijito vya Misri vitapungua
na kukauka.
Mafunjo na nyasi vitanyauka,
Copyright information for
SwhKC